UMEMSIKIA MANJI ALICHOSEMA JUU YA MILIONI 100 ZA SIMBA?

6:07 AM
Mwenyekiti wa Yanga, Yusuf Manji amesema amesikia kuna mtu ametoa Sh milioni 100 kuisaidia klabu moja na kuonekana ni mtu mwema Tanzania nzima.

Hali ambayo inamshangaza kwa kuwa kusaidia kwa upande wa Yanga tena kwa gharama ya juu ni jambo la kawaida kabisa.

Manji amesema hayo wakati wa mkutano wa dhararu wa wanachama aliouitisha kwenye Ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam, leo.

Ingawa Manji hajataja jina, lakini mfanyabiashara Mohammed Dewji alitoa Sh milioni 100 kusaidia usajili wa Simba.

“Nasikia wanasema ndiye tajiri namba moja Tanzania, ametoa Sh milioni mia kuisaidia klabu,” alisema Manji na wanachama wakashangilia.

Share this

SPORT HITS IS A BLOG BASED ON PROVIDING SPORT NEWS FROM ALL AROUND THE WORLD, STAY WITH US ALL THE TIME FOR INSTANT UPDATES.. Dont Forget to follow us on Facebook, twitter and Instagram @sporthitstz

Related Posts

Previous
Next Post »