MISRI KAMA ZALI MWANANGU| WATINGA FAINALI AFCON

3:31 PM
Timu ya Taifa ya Misri imefanikiwa kutinga Fainali ya michuano ya Afcon Nchini Gabon baada ya kuitoa timu ngumu ya Burkina Faso kwa changamoto ya mikwaju ya penati (4-3) baada ya kumaliza dakika 120 wakitoshana nguvu kwa kufungana goli 1-1 magoli yaliyofungwa kipindi cha pili Misri wakitangulia kufunga dakika ya 66 kupitia  kwa staa wake Muhamed Salah na kusawazishwa baada ya dakika saba kupitia kwa Bance.

Burkina Faco walionekana kuwa fiti zaidi baada ya kuwapeleka mchakamchaka Misri lakini walishindwa kumalizia mipira iliyokuwaikifika mara kwa mara langoni kwa Misri.
Sifa pekee zimuendee kipa mkongwe kuliko wote El Hedary ambae ameweka rekodi ya kucheza fainali hizo mara 7 huku akiwa na umri wa miaka 44mbaada ya kuokoa mikwaju miwili ya penati na kuipeleka Misri fainali.


Nusu fainali nyingine itachezwa kesho kwa kuikutanisha miamba miwili katika soka la Afrika Cameroon na Ghana.

Share this

SPORT HITS IS A BLOG BASED ON PROVIDING SPORT NEWS FROM ALL AROUND THE WORLD, STAY WITH US ALL THE TIME FOR INSTANT UPDATES.. Dont Forget to follow us on Facebook, twitter and Instagram @sporthitstz

Related Posts

Previous
Next Post »