FRANK LAMPARD ATANGAZA KUSTAAFU KUCHEZA SOKA

10:18 AM
                   
Mchezaji wa zamani wa Chelsea na timu ya Taifa ya Uingereza Frank Lampard ametangaza kustaafu kucheza soka. 
Lampard ambaye mkataba wake unaelekea ukingoni katika klabu ya New York City FC amesema hataongeza tena mkataba na wala hatosajili kwenye timu yoyote japo timu nyingi zimeonyesha nia ya kumuhitaji. 
Lampard amesema kwa sasa soka basi na anafungua ukurasa mpya wa maisha. 
Lampard ameitumikia Timu ya Taifa ya Uingereza kwa kuichezea mechi 106 ataenda kuaga katika klabu za Westham united, Manchester City na mwisho Chelsea klabu ambayo ameichezea kwa miaka 13.
Lampard mwenye umri wa miaka 38 amesema hatoweza kuisahau timu ya Chelsea kwa kumpa mafanikio makubwa kisoka. 

Share this

SPORT HITS IS A BLOG BASED ON PROVIDING SPORT NEWS FROM ALL AROUND THE WORLD, STAY WITH US ALL THE TIME FOR INSTANT UPDATES.. Dont Forget to follow us on Facebook, twitter and Instagram @sporthitstz

Related Posts

Previous
Next Post »