SUMAYE AFUTIWA HATI YA UMILIKI WA SHAMBA

9:51 AM
Waziri Mkuu mstaafu wa Tanzania Fredrik Sumaye amefutiwa hati miliki ya Shamba lake huko Bunju Jijini Dar es Salaam. 

Shamba hilo linaloingia mikononi mwa Serikali, ni lile liliko katika eneo la Mwabwepande jijini Dar es Salaam ambalo mwishoni mwaka jana, wananchi waliobomolewa nyumba zao ikidaiwa  walilivamia na kujenga.
Leo serikali imetangaza rasmi kufuta leseni ya eneo hilo.

Sumaye aliwahi kueleza kuwa ameliacha eneo kwani lengo lake ni kujenga chuo kikuu na sio vinginevyo. Aliweka wazi nia yake ya kufika mahakamani endapo atanyang’anywa eneo hilo.

Share this

SPORT HITS IS A BLOG BASED ON PROVIDING SPORT NEWS FROM ALL AROUND THE WORLD, STAY WITH US ALL THE TIME FOR INSTANT UPDATES.. Dont Forget to follow us on Facebook, twitter and Instagram @sporthitstz

Related Posts

Previous
Next Post »