JUMA ABDUL KUREJEA UWANJANI MWAKANI

12:53 AM
Beki wa Ynaga Juma Abdul huenda akakosekana kipindi chote kilichobaki kuelekea kualizika kwa mwaka 2016 kutokana na maumivu ya nyonga yanayomsumbua.
Kwa mujibu wa Daktari wa timu hiyo Edward Bavu, amesema Juma yupo chini ya uangalizi maalum ili kuhakikisha napata matibabu stahiki na kurejea mapema zaidi uwanjani.

“Kwa sasa tunaangalia maendeleo yake kabla ya kurudi uwanjani rasmi, kama akionekana bado ataendelea kukaa nje mpaka pale tutakaporidhika juu ya afya yake,” alisema Bavu.

Hata hivyo pamoja na daktari huyo kusema hivyo kumekuwa na hofu kubwa kuwa beki huyo hataweza kurudi uwanjani hadi Januari mwakani, kutokana na mechi tatu zilizobaki za mzunguko wa kwanza kuwa karibukaribu.

Yanga wanacheza na Mbeya City, halafu watavaana na Mbeya City wikiendi ijayo na mwisho watamaliza na Ruvu Shooting.

Mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu Bara unatarajiwa kumalizika Jumapili ijayo lakini viporo vitaenda hadi Novemba 13.

Share this

SPORT HITS IS A BLOG BASED ON PROVIDING SPORT NEWS FROM ALL AROUND THE WORLD, STAY WITH US ALL THE TIME FOR INSTANT UPDATES.. Dont Forget to follow us on Facebook, twitter and Instagram @sporthitstz

Related Posts

Previous
Next Post »