GEITA DISTRICT WASHINDWA KUTOKEA UWANJANI DHIDI YA MURUSAGAMBA KOMBE LA FEDERATION

5:46 AM
Timu ya Geita District ya Geita imeshindwa kutokea katika Dimba la kaitaba kucheza na Mabingwa wa Mkoa wa Kagera timu ya Murusagamba kutoka Ngara katika michuano ya Azam federation Cup ambayo ipo katika hatua za awali.
Timu ya Murusagamba imepata pointi za chee leo
Ilibidi waamuzi kuwasubiri kwa dakika 15 lakini timu ya Geita ilishindwa kutokea na ndipo mwamuzi wa pambano hilo alipopuliza kipenga kuashiria mchezo huo kumalizika.
Kwa mujibu wa kanuni za soka timu ya Murusagamba itapewa pointi 3 za mezani na magoli 2 na kusonga mbele katika michuano hiyo.

Kwa mujibu wa taarifa zilizopatikana kabla ya kumalizika kwa pambano hilo iliripotiwa Timu ya Geita ilipata tatizo la kiusafiri wakiwa njiani kuelekea kwenye mpambano huo.

Share this

SPORT HITS IS A BLOG BASED ON PROVIDING SPORT NEWS FROM ALL AROUND THE WORLD, STAY WITH US ALL THE TIME FOR INSTANT UPDATES.. Dont Forget to follow us on Facebook, twitter and Instagram @sporthitstz

Related Posts

Previous
Next Post »