AZAM FC YAIRARUA KAGERA SUGAR KAITABA

9:44 AM
Azam Fc imefanikiwa kujikusanyia pointi tatu muhimu baada ya kupata ushindi wa ugenini wa magoli 3-2 dhidi ya wenyeji wao Kagera Sugar katika mchezo uliochezwa leo katika dimba la Kaitaba.

Walikuwa Kagera Sugar waliotangulia kujipatia goli katika dakika ya 33  kupitia kwa mshambuliaji wake Themi Felix, Azam walicharuka na kufanikiwa kusawazisha dakika ya 40 goli likifungwa na kiungo mshambuliaji Mudathir Yahaya. Mpaka Timu zinakwenda mapumziko magoli yalikuwa ni 1-1.
Kipindi cha pili kilianza kwa kasi lakini walikuwa Kagera Sugar tena waliotangulia kwa kufunga goli la pili kupitia kwa mshambuliaji wake yuleyule Themi Felix aliyefunga goli dakika ya 68, 

Iliwalazimu Azam kusubiri mpaka dakika ya 81 kuweza kusawazisha goli hilo kupitia kwa Frank Domayo kabla ya nahodha wa Azam Jonh Bocco kuifungia Azam goli la Tatu na la ushindi katika dakika ya 86.

Share this

SPORT HITS IS A BLOG BASED ON PROVIDING SPORT NEWS FROM ALL AROUND THE WORLD, STAY WITH US ALL THE TIME FOR INSTANT UPDATES.. Dont Forget to follow us on Facebook, twitter and Instagram @sporthitstz

Related Posts

Previous
Next Post »