RUGE| JAPO NIMETUKANWA SANA, NAJIVUNIA KUUSOGEZA MUZIKI WA BONGO LEVO FULANI

11:28 AM
Mkurugenzi wa Uzalishaji wa Vipindi Clouds Media Group, Ruge Mutahaba amesema yeye ni mtu ambaye anaongoza kwa kutukanwa katika tasnia ya muziki kutokana na harakati zake za kuupigania muziki.

Akiongea Ijumaa hii katika semina ya wasanii wachanga wa Dodoma iliyofanyika katika Ukumbi wa Royal Village, Ruge amewataka wasanii hao kuacha kukata tamaa katika harakati wanazopitia.

“Mimi ni mtu ninaeongoza kwa kutukanwa kwenye tasnia ya muziki,” alisema Ruge. “Nimetukanwa sana lakini hilo haliniumizi, najivunia kwa kuwa tumepambana sana kuusimamisha muziki wetu hadi kufika hapa,”.

Ruge Mutahaba ni mmoja kati ya watu waliosaidia kwa namna moja kuchochea kukuwa kwa muziki wa bongofleva nchini licha ya baadhi ya watu kutokubali harakati zake.

Share this

SPORT HITS IS A BLOG BASED ON PROVIDING SPORT NEWS FROM ALL AROUND THE WORLD, STAY WITH US ALL THE TIME FOR INSTANT UPDATES.. Dont Forget to follow us on Facebook, twitter and Instagram @sporthitstz

Related Posts

Previous
Next Post »