Kambi rasmi ya upinzani sasa inaukumbuka na kuuthamini utawala wa aliyekuwa Spika wa Bunge lilopita Anne Makinda kwa kuwa alitumia sana Hekima na Busara kutatua tofauti mbalimbali zilizojitokeza ndani ya ukumbi wa Bunge.
"Makinda alikuwa akiuona mmeenda kinyume tu, anawaandikia kimemo mbunge mmoja mmoja akiwataka mkutane ofisini kwake na kuyamaliza. Hakukuwa na mwanya wa kushindana tofauti na Dr. Tulia." Amesema Kaimu kiongozi wa Kambi ya Upinzani, David Silinde.
Amesema mgawanyiko uliopo sasa baina ya wabunge wa Chama Tawala na kile cha Upinzani unatokana na kukosekana kwa Spika Job Ndugai kwa muda mrefu.
EmoticonEmoticon