STARS YAKUBALI KICHAPO NYUMBANI, WAMISRI WAFUZU AFCON

9:18 AM
Kiungo wa AS Roma Muhamed Salah leo amezima matumaini ya Tanzania kushiriki kwa mara ya pili michuano ya AFCON baada ya kutupia magoli mawili peke yake katika dakika za 43 na 58, 
Salah aliyekuwa mwiba kwa stars leo alifunga goli la kwana dakika ya 43 kwa mpira wa adhabu nje kidogo ya lango la Stars na kupiga mpira uliomshinda Aishi manula na kuingia mojakwamoja golini.
                                  Muuaji wa Stars Mohamed Salah
Kpindi cha pili kilianza kwa Timu zote kushambuliana kwa zamu na Taifa Stars kufanikiwa kupata penati ambayo ilipaishwa juu na Mbwana Samatta na baadae Salah kuongeza goli la pili baada ya kuwazidi ujanja na nguvu viungo na mabeki wa Stars hadi mwisho wa Mchezo Tanzania 0-2 Misri 
Kwa matokeo hayo Misri iliyokamilisha michezo yake kwa kujikusanyia pointi 10 inafuzu kwenye michuano ya AFCON na kuziacha Tanzania na Nigeria zikisuburi kumalizia mchezo wao wa mwisho wa kukamilisha ratiba utakaochezwa Nigeria.



Share this

SPORT HITS IS A BLOG BASED ON PROVIDING SPORT NEWS FROM ALL AROUND THE WORLD, STAY WITH US ALL THE TIME FOR INSTANT UPDATES.. Dont Forget to follow us on Facebook, twitter and Instagram @sporthitstz

Related Posts

Previous
Next Post »