MASTER JAY ATANGAZA KURUDI KWENYE GAME YA MUZIKI

1:08 AM
Mtayarishaji mkongwe wa muziki nchini, Master J ametangaza habari njema ya kurudi kwenye kutayarisha wa muziki baada ya kupumzika kwa miaka kadhaa.


Akizungumza na chanzo kimoja cha habari Jumanne hii, Master J amesema ameamua kusikiliza maombi ya mashabiki wake ambao wamekuwa wakimtaka arudi kwenye game kwa muda mrefu.

“Watu wamenishawishi sana lakini nafikiria, hata Majani tumeongea kwa marefu na naweza sema labda mwaka huu nitarudi, nitakumbushia kumbushia kazi kigogo,” alisema Master J.

Pia mtayarishaji huyo alisema watayarishaji wa muziki wa sasa wananufaika zaidi na kazi zao tofauti na wao ambao walianza kwa kufanya kazi nyingi za bure.

Share this

SPORT HITS IS A BLOG BASED ON PROVIDING SPORT NEWS FROM ALL AROUND THE WORLD, STAY WITH US ALL THE TIME FOR INSTANT UPDATES.. Dont Forget to follow us on Facebook, twitter and Instagram @sporthitstz

Related Posts

Previous
Next Post »