Comment ya Zitto Kabwe baada ya Rais Magufuli kumfuta kazi Charles Kitwanga

5:05 PM
Stori kubwa ambayo imeingia kwenye headlines jioni ya May 20 2016 lakini pia inatarajiwa ndio itakaa katika kurasa za mbele za magazeti ya kesho May 21 2016, ni kuhusu uamuzi wa Rais Magufuli kumfuta kazi aliyekuwa waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Charles Kitwanga kutokana na kuingia bungeni akiwa amelewa.

Mbunge wa Kigoma Mjini na kiongozi wa chama cha ACT Wazalendo Zitto Kabwe ametumia ukurasa wake wa facebook kuandika mtazamo wake baada ya Rais Magufuli kufanya maamuzi hayo ya kumfuta kazi waziri Kitwanga.

“Uamuzi wa Rais kumfukuza kazi Waziri wa Mambo ya Ndani unatuma ujumbe mmoja – hataki mchezo. Rais amethibitisha kuwa anao uwezo wa kutumbua hata aliowateua. Ni maamuzi muhimu sana kwa Kiongozi wa aina yake. Wale vijana waliokuwa wanatumwa kumtetea wasimame kumtetea. Rais kaonyesha Uongozi ‘ no nonsense “
 

Ujumbe wa aliyouandika Zitto Kabwe baada ya Rais Magufuli kumfuta kazi aliyekuwa waziri wa mambo ya ndani ya nchi Charles Kitwanga

Share this

SPORT HITS IS A BLOG BASED ON PROVIDING SPORT NEWS FROM ALL AROUND THE WORLD, STAY WITH US ALL THE TIME FOR INSTANT UPDATES.. Dont Forget to follow us on Facebook, twitter and Instagram @sporthitstz

Related Posts

Previous
Next Post »