SIMBA YARUDI KIELENI

10:56 AM
 Timu ya Simba imefanikiwa kurudi kileleni mwa ligi kuu ya Tanzania Bara baada ya kuifunga timu ya Tanzania prison Kwa magoli 3-0. Katika mtanange huo timu ya Simba ilitawala vipindi vyote viwili vya mchezo huo huku James Kotei na Ndemla wakiikamata vizuri sehemu ya kiungo na kuwadhibiti vilivyo wachezaji wa Prison.
Mchezaji kutoka zesco ya Zambia anaeichezea klabu ya Simba Kwa mkopo alikuwa wa kwanza kuifungia goli Timu ya Simba baada ya kuumalizia krosi ya beki wa Simba Javier Bukungu dakika ya 18.
Dakika ya 28 Ibrahim Ajib aliwainua tena wana msimbazi Kwa kupachika goli la pili akimalizia pasi aliyosetiwa na Laudit Mavugo. . Mpaka timu zinakwenda mapumziko Simba Ilikuwa inaongoza Kwa magoli 2-0.
kipindi cha pili kilianza kwa kasi lakini walikuwa ni Simba waliofanikiwa kupata goli la tatu kupitia kwa Laudit Mavugo katika dakika ya 68.
Kwa matokeo hayo Simba imefikisha alama 51 mbili mble ya Yanga na kurudi katika nafasi ya kwanza waliokuwa wakiishikilia kwa nuda mrefu kabla ya kunyang'anywa na Yanga ambao bado wana mchezo mmoja mkononi.

Share this

SPORT HITS IS A BLOG BASED ON PROVIDING SPORT NEWS FROM ALL AROUND THE WORLD, STAY WITH US ALL THE TIME FOR INSTANT UPDATES.. Dont Forget to follow us on Facebook, twitter and Instagram @sporthitstz

Related Posts

Previous
Next Post »