MICHUANO ya Kombe la Mapinduzi inaanza rasmi leo kwa mechi mbili za Kundi A kuchezwa Uwanja wa Amaan, Zanzibar.
Wenyeji KVZ watamenyana na mabingwa watetezi, URA kuanzia Saa 10:00 jioni, kabla ya vinara wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, Simba kumenyana na Taifa Jang'ombe kuanzia Saa 2:30 usiku.
Mechi za Kundi B zitaanza kesho kwa Azam kucheza na Zimamoto kuanzia Saa 10:00 jioni, kabla ya mabingwa wa Tanzania Bara, Yanga kumenyana na Jamhuri ya Pemba kuanzia Saa 2:30 usiku.

EmoticonEmoticon