MAMIA YA WAMAREKANI WAANDAMANA KUPINGA USHINDI WA TRUMP

2:44 AM
Kufuatia kutangazwa kwa Donald Trump kuwa Rais mteule wa Marekani, wananchi wa Marekani wameandamana katika miji saba kupinga ushindi huo wa Trump.
Waandamanaji hao wamekusanyika nje ya mnara maarufu wa Trump ‘ Trump Tower’ mjini New York wakipaza sauti za kumpinga Trump. Wengine walionekana nje ya Ikulu ya Marekani wakipaza sauti kuwa “Not my president” (Si Rais wangu), pamoja na mabango mengine.
Wengi wa waandamanaji walioongea na CNN wameelezea kuwa wana wasiwasi sana kuhusu Trump kwavile kuongoza Marekani sio kama kuiongoza nchi yoyote duniani.
“Kwa matokeo haya tumeiangusha Dunia. Trump hakustahili kuwa Rais. Nahisi watu walipiga kura kwa hasira lakini Trump ni hatari kwa dunia,” alisema mmoja wa waandamanaji aliyejitambulisha kwa jina la James Betwell kutoka Califonia.

Share this

SPORT HITS IS A BLOG BASED ON PROVIDING SPORT NEWS FROM ALL AROUND THE WORLD, STAY WITH US ALL THE TIME FOR INSTANT UPDATES.. Dont Forget to follow us on Facebook, twitter and Instagram @sporthitstz

Related Posts

Previous
Next Post »