PICHA: Tunda Man aachana na ukapela| Afunga Ndoa Morogoro

11:01 AM
MWANAMUZIKI wa kizazi kipya nchini kutoka kundi la TipTop Connection, Tunda Man amefunga ndoa na mchumba wake wa muda mrefu Bi Sabra, ndoa ya wawili hao imefungwa kwenye Msikiti Mkuu wa barabara ya Boma, mjini Morogoro.

Mkali huyo wa wimbo uitwao ‘Mama Kijacho’ amefunga ndoa hiyo siku ya jana Ijumaa na kuhudhuriwa na baadhi ya marafiki zake wa karibu akiwemo Madee, Dogo Janja na Kassim Mganga. Kabla ya ndoa hiyo kufungwa ilitanguliwa na sherehe ya kuagwa binti ‘Send-off’ iliyofanyika juzi alhamisi.
Kwa mujibu wa shuhuda wetu aliye mjini Morogoro, sherehe hiyo ya harusi inaendelea kwa siku ya tatu leo nyumbani kwa bibi harusi.





Share this

SPORT HITS IS A BLOG BASED ON PROVIDING SPORT NEWS FROM ALL AROUND THE WORLD, STAY WITH US ALL THE TIME FOR INSTANT UPDATES.. Dont Forget to follow us on Facebook, twitter and Instagram @sporthitstz

Related Posts

Previous
Next Post »