MWAMBUSI KUSHIKA USUKANI KWA MUDA BAADA YA PLUIJM KUJIUZULU

9:20 AM
Kocha Msaidizi wa Yanga, Juma Mwambusi atakiongoza kikosi cha Yanga katika mechi zilizobaki hadi hapo kocha mkuu mpya atakapoanza kazi.
Taarifa za ndani kutoka Yanga zinasema George Lwandamina raia wa Zambia ataanza kazi rasmi Novemba Mosi.
Tayari Lwandamina yuko jijini Dar es Salaam na Kocha Hans van der Pluijm ameachia ngazi rasmi kuinoa Yang.
“Mwambusi ndiye ataendelea na kikosi, mambo mengine yakikamilika Lwandamina ataanza kazi,” alisema.

Awali ilielezwa kwamba Pluijm atakuwa ni Mkurugenzi wa Ufundi wa Yanga kabla ya mwenyewe kuamua kujiuzulu.

Share this

SPORT HITS IS A BLOG BASED ON PROVIDING SPORT NEWS FROM ALL AROUND THE WORLD, STAY WITH US ALL THE TIME FOR INSTANT UPDATES.. Dont Forget to follow us on Facebook, twitter and Instagram @sporthitstz

Related Posts

Previous
Next Post »