TBL WAICHINJIA BAHARINI SIMBA SC.

5:46 AM
Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), imeamua kutosaini mkataba wa kuendelea kuidhamini Simba.

Taarifa kutoka ndani ya Simba, zinaeleza TBL imegoma kusaini mkataba ikionekana kuingia hofu baada ya Yanga kutotaka kuendelea nao au waingie wakiwa na ofa mpya.

“TBL wameona Yanga wanataka vitu vingi sana na kwao haitakuwa na faida, hivyo wameachana nao.

“Simba hawana shida, lakini watasaini vipi na Simba wakati kawaida zinatakiwa timu zote,” kilieleza chanzo.
“Hivyo wameamua kujiondoa na mkataba wao unaisha keshokutwa Jumapili.





“Sasa hili ni tatizo katika ulipaji mishahara kwa Simba maana lazima ugumu utaongezeka,” kilisisitiza chanzo.




Pamona na hivyo imeelezwa kumekuwa na juhudi binafsi zinazofanywa na baadhi ya viongozi kujaribu kuwashawishi TBL kupitia Kilimanjaro, wabadili uamuzi.

Share this

SPORT HITS IS A BLOG BASED ON PROVIDING SPORT NEWS FROM ALL AROUND THE WORLD, STAY WITH US ALL THE TIME FOR INSTANT UPDATES.. Dont Forget to follow us on Facebook, twitter and Instagram @sporthitstz

Related Posts

Previous
Next Post »