OMONG AANZA KWA KISHINDO MSIMBAZI, POLISI WALA VIRUNGU 6-0| Mu Ivory Coast kama kawa

9:51 AM
Hatimaye Kocha Joseph Omog ameanza kukiona kikosi chake kikicheza mechi ya kwanza ya kirafiki na kushinda kwa mabao 6-0 dhidi ya Polisi inayoshiriki Ligi Daraja la Kwanza.

Katika mechi hiyo iliyopigwa katika Uwanja wa Chuo cha Biblia cha Highlands cha Morogoro, Simba walionyesha soka safi na la kuvutia.


Raia wa Ivory Coast, Fredric Blagnon ameanza vizuri kwa kupachika mabao mawili sawa na yale ya Ibrahim Ajib.

Wengine waliofunga mabao ni Abdi Banda na Mohammed Mussa Kijiko.

Hiyo ni mechi ya kwanza ya Simba ya kirafiki na ya kwanza kupata ushindi mnono, jambo ambalo litainua morali zaidi ya Msimbazi.

Share this

SPORT HITS IS A BLOG BASED ON PROVIDING SPORT NEWS FROM ALL AROUND THE WORLD, STAY WITH US ALL THE TIME FOR INSTANT UPDATES.. Dont Forget to follow us on Facebook, twitter and Instagram @sporthitstz

Related Posts

Previous
Next Post »