MARTIAL ACHUKIZWA NA KITENDO CHA KLABU YAKE KUMNYANG'ANYA JEZI NAMBA 9

9:47 PM
Katika kile kinachoonekana ni kutofurahishwa na kitendo cha kunyang'anywa jezi yake namba 9 na kupewa Ibrahimovic, straika wa Manchester United Anthony Martial ameamua ku unfollow account zote za jamii zinazomilikiwa na klabu hiyo zikiwemo Instagram,Facebook na Twitter.
Mabosi wa Manchester United walikubaliana na Ibrahimovic aliyetua Manchester akitokea klabu ya Paris st German ya nchini Ufaransa kuvaa jezi hiyo baada ya yeye mwenyewe kuhitaji namba hiyo ya Martial na kukubaliwa bila kipingamizi.
Kwa mujibu wa habari kutoka RMC Sporsts Manchester United hawakumpa taarifa Martial juu ya jambo hilo bali walifanya maamuzi bila kumshirikisha na kuzua sintofahamu baina ya mchezaji huyo na klabu yake.

Share this

SPORT HITS IS A BLOG BASED ON PROVIDING SPORT NEWS FROM ALL AROUND THE WORLD, STAY WITH US ALL THE TIME FOR INSTANT UPDATES.. Dont Forget to follow us on Facebook, twitter and Instagram @sporthitstz

Related Posts

Previous
Next Post »