MAANDAMANO YAPO KAMA YALIVYOPANGWA-CHADEMA

9:27 PM
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesisitiza kuendelea na dhamira yake ya kufanya maandamano nchi nzima ifikapo Septemba Mosi, mwaka huu licha ya Rais John Magufuli kutoa tahadhari dhidi ya kitendo hicho leo alipokuwa akihutubia mkutano wa hadhara mkoani Singida.

Hayo yamesemwa usiku huu na Katibu Mkuu wa chama hicho, Dk Vicent Mashinji katika kipindi cha Mada Moto kinachorushwa na kituo cha Televisheni cha Channel Ten jijini Dar es Salaam.

“Lengo letu tunataka kuwaeleza wananchi hasa wanachama wa chama chetu maazimio tuliyokubaliana katika mkutano wetu uliomalizika hivi karibuni,” amesema Dk Mashinji.

Amesema Chadema hawakusudii kufanya vurugu bali watafanya maandamano ya amani yanayolenga kwenda kupokea taarifa ya mkutano.

“Nashangaa ni kwanini maandamano haya yanawatia hofu watawala kiasi cha kutaka kuyazuia na wala hatuhitaji ulinzi wa polisi, tutaenda kwa amani tu,” amesema katibu mkuu huyo.
Chanzo:Mwananchi

Share this

SPORT HITS IS A BLOG BASED ON PROVIDING SPORT NEWS FROM ALL AROUND THE WORLD, STAY WITH US ALL THE TIME FOR INSTANT UPDATES.. Dont Forget to follow us on Facebook, twitter and Instagram @sporthitstz

Related Posts

Previous
Next Post »