Rais Magufuli aijibu kampeni ya kuziba midomo ya wabunge wa upinzani

8:59 AM
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt John Pombe Magufuli ameijibu kampeni iliyoanzishwa na upinzani ya kuziba midomo yao kudai kuwa serikali ya awamu ya tano imekosa demokrasia.
Alikuwa akihutubia Alhamis hii ikulu jijini Dar es Salaam wakati wa kukabidhiwa ripoti ya uchaguzi uliopita.

“Niwaombe wanasiasa wenzangu, ushindani wa sasa hivi wa vyama vya siasa ambao unatakiwa upigiwe nguvu zaidi ni kwa wale wawakilishi waliopewa mamlaka na wananchi. Kama ni kwa madiwani wakapeleke hoja kwa nguvu sana kwenye maeneo yao,” alisema.

“Kama ni wabunge wakazungumze kwa nguvu zote bungeni lakini hata kuziba midomo nayo ni demokrasia,” aliongeza na kusababisha kicheko kwenye ukumbi wa ikulu jijini Dar.

“Kwahiyo hiyo ndio demokrasia ya muelekeo ya aina yake.”

Share this

SPORT HITS IS A BLOG BASED ON PROVIDING SPORT NEWS FROM ALL AROUND THE WORLD, STAY WITH US ALL THE TIME FOR INSTANT UPDATES.. Dont Forget to follow us on Facebook, twitter and Instagram @sporthitstz

Related Posts

Previous
Next Post »