ITALY YAIADHIRI SPAIN, Spain wakubali kichapo na kuutema rasmi ubingwa wa Euro

12:41 PM
Timu ya Taifa ya Italia imeivua rasmi ubingwa Timu ya Taifa ya Hispania kwa kuifunga jumla ya magoli 2-0 katika hatua ya mtoano ya 16 bora.
Giorgio Chiellini akishangilia goli lake

Giorgio Chiellini alianza kuifungia Italia dakika ya 33  ya mchezo. 
Wakati mashabiki na pengine hata wachezaji wakiamini huenda mechi itaisha kwa goli hilo moja dakika ya 90 Graziano Pelle aliifungia Italia goli la pili na kuipa mkono wa kwaheri Hispania ambae ndio alikuwa bingwa mtetezi.
Kwa matokeo hayo Italia atakutana na Ujerumani katika hatua ya Robo Fainali.
Baada ya miaka 8 ya utawala wa Ulaya hatimae Hispania imeaga rasmi mashindano ya mwaka huu nhini Ufaransa.
Pelle akifunga goli la pili kwa Italia

Share this

SPORT HITS IS A BLOG BASED ON PROVIDING SPORT NEWS FROM ALL AROUND THE WORLD, STAY WITH US ALL THE TIME FOR INSTANT UPDATES.. Dont Forget to follow us on Facebook, twitter and Instagram @sporthitstz

Related Posts

Previous
Next Post »