DORTMUND WAKATAA OFA YA EURO 19M KUTOKA KWA MANCHESTER KUMNYAKUA HENRIKH MKHITARYAN

3:18 PM

Klabu soka ya Dortmund ya Nchini Ujerumani imekataa ofa ya Euro 19 M kutoka kwa Manchester United ya Uingereza ofa iliyolenga kumnyakua kiungo wa Brossia Dortmund Henrikh Mkhitaryan.

Wajerumani hao wamesisitiza hawana mpango wa kumuuza kiungo huyo ambae ametoa mchango mkubwa sana kwa Timu hiyo msimu uliyopita kwa kupachika magoli 18 na kutoa pasi za magoli 20 katika jumla ya mashindano yote aliyocheza akiwa na Dortmund.


Kiungo huyo aliyebakiza mwaka mmoja kwenye mkataba wake alikuwa anawindwa pia na klabu za Arsenal na Chelsea lakini kwa mujibu wa Agenti wake Mino Raiola amesema mteja wake alipendelea zaidi kutua katika klabu ya Manchester United.

Licha ya Henrikh Mkhitaryan kukataa kuongeza mkataba Dortmund bado wanashikilia msimamo wao wa kutokumuuza kiungo huyo wakiamini ni mtu muhimu kwao na bado wanahitaji huduma yake

Share this

SPORT HITS IS A BLOG BASED ON PROVIDING SPORT NEWS FROM ALL AROUND THE WORLD, STAY WITH US ALL THE TIME FOR INSTANT UPDATES.. Dont Forget to follow us on Facebook, twitter and Instagram @sporthitstz

Related Posts

Previous
Next Post »